Serikali kushughulikia malalamiko ya korosho


Daudi Manongi, MAELEZO, Dodoma

Mikorosho mashambani
SERIKALI itashughulikia malalamiko ya wakulima wa korosho kwa kuondoa makato yasiyo muhimu kwenye zao hilo.

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William ole Nasha alibainisha hayo wakati akijibu maswali ya wabunge jana akiahidi kuwa Serikali itatekeleza hilo.

“Serikali imeshafanyia marekebisho maeneo ambayo wakulima walikuwa wanalalamikia kwa kuondoa makato hayo kwenye zao hilo,” alisema Ole Nasha.

Alisema Serikali imefuta ushuru wa Sh 20 kwa kilo kwa ajili ya Chama Kikuu cha Ushirika, Sh 50 za usafirishaji korosho, Sh 10 kwa kilo kwa ajili ya mtunza ghala na Sh 10 kwa kilo kwa ajili ya kikosikazi cha masoko.

Alisema sekta ya korosho ina utaratibu wa kupanga beidira kwa kutumia vigezo vinavyokubaliwa kwa pamoja na wadau wote.

Kwa upande wa ununuzi wa pembejeo, alisema hufanywa kwa pamoja na vyombo rasmi ndani ya sekta hiyo ambapo awali ilikuwa ikisimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Korosho na sasa Bodi ya Korosho Tanzania.

Alieleza changamoto zinazojitokeza katika kufikisha pembejeo hizo kwa wakulima wa korosho na kwamba hatua zimechukuliwa kwa kushirikisha vyama vya ushirika ili kudhibiti mianya ya pembejeo kwenda kwa wasiolengwa.

Kwa mujibu wa Ole Nasha, Serikali imeweka mfumo wa usambazaji pembejeo kwa lengo la kuhakikisha pembejeo hizo zinafikia walengwa pekee.

“Utaratibu huu unazingatia kutambua wakulima wenye uhitaji na pembejeo na hununuliwa kwa utaratibu wa ununuzi wa pamoja na kusambazwa kwa wakulima kupitia wakala  walioteuliwa na kuthibitishwa na Halmashauri husika,” alisisitiza Ole Nasha.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo