Washauriwa kushirikiana na Wachina


Mwandishi Wetu

KAMPUNI za ujenzi nchini zimeshauriwa kuungana na kushirikiana na za China ili kujifunza namna wanavyofanya kazi kwa ufanisi.

Rai hiyo ilitolewa jana Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Asasi ya Ushirikiano kati ya Tanzania na China, Joseph Kahama, akisema kampuni za ujenzi nchini bado zina safari ndefu ya kuongeza ujuzi na mbinu za kibiashara.

“Kujifunza kuna njia nyingi ni utaratibu mzuri kujipanga kibiashara kwani ni muhimu kuelewa kwamba zaidi ya asilimia 80 ya kampuni kubwa za ujenzi duniani zinatoka China, na nchini zipo nyingi kwa sasa, hivyo huu ndio wakati wetu wa kuchota ujuzi,” alisema Kahama.

Alifafanua, kwamba Wachina ndio wanaongoza katika ujenzi duniani na mataifa mbalimbali  yaliyoendelea kampuni za kichina ndizo zilizosimamia majengo yao, hivyo kampuni za nchini haziwezi kukwepa zikitaka kufanikiwa wajipenyeze na kuomba ushirikiano kwa Wachina na watajifunza mengi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC East Africa Limited), Yigao Jiang alisema kampuni yake imekuwa nchini tangu miaka ya 60 na wako tayari kusaidia Watanzania katika nyanja zote yakiwamo masuala ya kijamii.

“Mbali ya kushiriki ujenzi wa magorofa na miundombinu, kampuni yetu inaguswa na matatizo ya kijamii kwa sababu Watanzania ni ndugu zetu sasa, tumeshiriki ujenzi wa reli ya Tazara, tumejenga jengo la Ushirika (Mnazi Mmoja), tumejenga jengo la Nasaco (Dar es Salaam).

Alisema: “Vilevile jengo la ukumbi mpya Ikulu, Dar es Salaam tumeshiriki kuujenga na sasa tunajenga makutano ya barabara za juu Ubungo.”

Kuhusu fursa zinazopatikana kutokana na kampuni za ujenzi za China, Kahama alisema: “Watanzania wanapata ajira kwa sababu wasimamizi ni Wachina, lakini wafanyakazi wanatoka hapahapa, vilevile wananunua mchanga, saruji, kokoto, nondo na vifaa vingine vya ujenzi nchini.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo