Ukatili kijinsia waendelea soko la Feri


Dotto Mwaibale

Soko la Feri
ENEO la Lebanon katika soko la kimataifa la samaki la Feri, Dar es Salaam, limeelezwa kuongoza kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia hasa dhidi ya watoto.

Hayo yalielezwa na Mwenyekiti wa Soko hilo, Ali Bunda alipozungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati akitoa taarifa ya kupungua kwa ukatili wa kijinsia katika soko hilo baada ya kupata mafunzo kutoka Shirika la Equality for Growth (EfG).

"Vitendo vya ukatili wa kijinsia vimepungua kwa kiasi kikubwa katika maeneo mengine ya soko letu, lakini changamoto kubwa ipo Lebanon, huko ukipita usiku unaweza kulia kutokana na vitendo vinavyofanyika," alisema Bunda.

Alisema katika eneo hilo kila vitendo vichafu vimekuwa vikifanyika kwani hivi karibuni kuna mwanamume alikamatwa akimlawiti mtoto wa kiume na alipofikishwa kituo cha Polisi mtoto huyo aliomba mwanamume huyo asipelekwe mahakamani, kwani ni msaada mkubwa kwake kwa kuwa amekuwa akimpa fedha za chakula na mahitaji mengine.

"Kauli ya mtoto huyo ilimshitua kila mtu aliyekuwa kituoni hapo lakini pamoja na maombi hayo, polisi waliendelea kumshikilia ili sheria ichukue mkondo wake," alisema Bunda.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo