Vifaa vya kufundishia Sayansi vyapokewa


Said Mwishehe

Profesa Joyce Ndalichako
SERIKALI imetatua changamoto ya vifaa vya kufundishia masomo ya Sayansi katika sekondari za kata baada ya kuingiza kontena 17 za vifaa vyenye thamani ya Sh bilioni 16.9. Vifaa hivyo vitaanza kusambazwa leo kwenye sekondari hizo na chini ya Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Akizungumza jana Dar es Salaam wakati akipokea vifaa hivyo, Kaimu Kamishna wa Elimu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Nicolas Buretta, alisema anaamini wanafunzi watajifunza Sayansi kwa vitendo, kwani vifaa hivyo ni vya kutosha.

“Wizara tumepokea vifaa vya kufundishia masomo ya Sayansi kutoka kampuni ya Lab Equip Ltd ambayo ilishinda zabuni hii.

“Pia tumewaomba JWTZ kuvisambaza kwenye sekondari zote za kata zilizokamilisha maabara. Tunatarajia usambazaji huu utakamilika mwezi huu,” alisema Buretta.

Alifafanua kuwa changamoto ya uhaba wa vifaa vya kufundishia masomo ya Sayansi imekuwa ya muda mrefu, lakini sasa imefika mwisho baada ya kuanza kuwasili kwa kontena 17 za vifaa hivyo.

Wakati huo huo, alisema ili kukabiliana na uhaba wa walimu wa Sayansi, Wizara imeomba kibali cha kuajiri walimu 3,104 ili kupunguza uhaba huo.

Alisema lengo ni walimu 4,129 lakini waliamua kujiridhisha kwa sifa za walimu hao na kufanikiwa kupata walimu 3,104 wenye sifa stahiki na ndio watakaoajiriwa.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo