Wanawake washika uongozi sokoni


Dotto Mwaibale

WAFANYABIASHARA wanawake kwenye masoko jijini Dar es Salaam wamejitambua na kujitokeza kugombea uongozi katika maeneo yao ya biashara.

Hayo yamebainishwa na Mwezeshaji wa Kisheria katika Soko la Tabata Muslim, Irene Daniel wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam kuhusu faida waliyopata kutokana na  mafunzo ya kupinga ukatili wa kijinsia sokoni kupitia Shirika la Equality for Growth (EfG)

"Kwa kweli wanawake hivi sasa tuko imara, tunajitambua na tuna uthubutu baada ya kupata dozi kutoka EfG kwani hapo awali tulikuwa waoga na hatukujua haki zetu ndiyo maana tulikuwa nyuma kimaendeleo," alisema Irene.

Alisema baada ya mafunzo hayo na kuwezeshwa kujua sheria na mambo yaliyokuwa yakimdhalilisha mwanamke, hali ni shwari katika masoko kwani hivi sasa wanafanya biashara zao katika mazingira salama.

Alisema kutokana na hali hiyo wanawake wamejitokeza kugombea uongozi na kuwa wajumbe katika kamati za masoko jambo ambalo ni la kujivunia.

Mfanyabiashara mwingine kwenye soko hilo ambaye pia ni Mwezeshaji wa Kisheria, Aisha Juma alisema taaluma waliyopata kupitia EfG imesaidia kuweka mambo sawa na ushirikiano baina yao kwenye masoko kwani leo hii hakuna mtu wa kumnyanyasa mwenzake kutokana na jinsia yake na anayebainika amekuwa akichukuliwa hatua.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo