CUF Tanga waanza kushiriki vikao


Ibrahim Kunoga, Tanga

Mussa Mbarouk
MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CUF), Mussa Mbarouk, amefichua siri ya madiwani wa chama hicho kulegeza msimamo wao na kuamua kuingia kwenye vikao vya Baraza la Halmashauri ya Jiji hilo.

Sababu kubwa ya kulegeza msimamo wao ni baada ya kupewa baraka na Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Shariff Hamad.

Akizungumza katika mkutano wake wa kwanza wa hadhara uliofanyika uwanja wa Tangamano,Mbunge huyo ambaye awali alikuwa amezuiwa kufanya mikutano hiyo alisema Katibu wa o mkuu ndiye aliyetoa baraka ili kusukuma maendeleo ya wananchi.

“Katibu wetu mkuu alituita na kuwataka madiwani wa Jiji la Tanga kuingia katika vikao vya baraza kwa sababu kuendelea kugoma ni kusababisha kudodora maendeleo ya wananchi,” alisema Mbarouk.

Alisema katika kipindi cha mwaka mmoja ambacho madiwani wa CUF waligoma kuingia katika vikao vya baraza hilo, miradi mingi ilikwama na kama wasingebadili msimamo, Benki ya Dunia ingesitisha msaada wa zaidi ya dola za Marekani milioni 500.

Mbunge huyo alisema katika kipindi kifupi ambacho madiwani hao kukubali kuhudhuria vikao, miradi mingi ya maendeleo imeanza kutekelezwa ikiwamo ujenzi wa barabara za mitaa kwa kiwango cha lami.

“Tanga tumeamua kuacha tofauti zetu za vyama, madiwani tumeungana kwa ajili ya maendeleo na tunataka Tanga ikimbie,” alisema mbunge.

Awali, madiwani wa kata mbalimbali walieleza miradi iliyotekelezwa katika maeneo yao na mikakati iliyopo ya kuhakikisha sekta ya elimu, afya, maji, barabara na masuala ya kijamii inaendelezwa.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo