Jengo la familia ya Mange kuuzwa


Suleiman Msuya

Mange Kimambi
JENGO maarufu la kampuni ya Triz Motel Limited linalodaiwa kumilikiwa na familia ya Mtanzania aishiye Marekani, Mange Kimambi ni miongoni mwa nyumba na viwanja 10 vilivyotangazwa kuuzwa kwa mnada na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Katika tangazo lake la juzi la mnada utakaofanywa na Wakala wa Serikali, Kampuni ya Msolopa, Wizara hiyo iliwataka wananchi kujitokeza kununua mali hizo za wadaiwa.

Mange aliyejipatia umaarufu kwa kuwa mchangiaji na mkosoaji wa mwenendo wa Serikali ni mtoto wa marehemu John Kimambi ambaye anatajwa kuwa mmiliki wa nyumba hiyo iliyoko Kinondoni.

Katika mnada huo ambao unatarajiwa kufanyika Machi 25 hadi Aprili mosi unahusu pia wadaiwa Highland Estates Limited, Universal Electronics and Hard Work, Bingo Simba Magwila, Zein Mohamed Baharoon na Camel Developers (T) Limited ambaye anadaiwa viwanja vitano.

Wadaiwa hao wanamiliki viwanja namba 479 Mbezi, 102 Mbezi, 46/1A/C Pugu , 2165 Mbezi , 79 na 86 Gerezani, 40 Kimbiji, 12-58 Temeke Mwanamakuru, 11 Mwanamakuru, 22 Aman Gomvu na 21 Aman Gomvu.

Kulingana na tangazo hilo, mnunuzi atapaswa kulipa asilimia 25 baada ya nyundo ya dalali na salio kulipwa ndani ya siku 14 huku anayeshindwa kulipa akipoteza haki na gharama za kuhamisha ununuzi zitakuwa juu ya mnunuzi.

Akizungumzia kiwanja hicho kwenye mitandao ya kijamii, Mange alidai Magufuli (Rais John) ameamua kuuza eneo lake la familia ambalo anamiliki asilimia 25 ya hisa.

Alisema familia yake haijui kuhusu deni linalohusishwa na nyumba hiyo na kwamba yeye ndiye aliwaambia ndugu zake kwa ujumbe kuwa nyumba yao inauzwa “Eti tunadaiwa ardhi,” alisema na kuongeza: “Yaani ni kichekesho cha mwaka … hawana barua hata moja ya kuambiwa wakalipe chochote Ardhi.

Na nilihakikisha wanalipa kodi vizuri ili tusimpe sababu.” Kupitia mitandao ya kijamii Mange aliandika: “Wewe uza mpaka nyumba za babangu zote, fanya lolote lile muhimu tu utaniacha ….”
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo