DC Temeke ahimiza kuepuka kipindupindu


Dalila Sharif

Felix Lyaniva
MKUU wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaniva, ametaka wananchi wa wilaya hiyo kuwa waangalifu na wajiepushe na ulaji ovyo ili kuepuka magonjwa hatarishi kama kipindupindu.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi juzi Dar es Salaam, Lyavina alisema kutokana na ongezeko la uuzaji na matumizi ya vyakula kwenye mazingira hatarishi, ni vema kila mwananchi akazingatia usafi wa mazingira maeneo ya kazi hata katika uuzaji bidhaa za vyakula wilayani humo.

Alisema hali hiyo itasaidia kupunguza magonjwa hatarishi kikiwamo kipindupindu hivyo kuokoa maisha ya watu.

“Kipindupindu ni cha mlipuko, kinatokea wakati wowote kutokana na mazingira kuwa hatarishi hasa katika kipindi hiki cha mvua,” alionya Lyaniva.

Alisema uhifadhi na ununuaji wa vyakula salama utasaidia kupunguza magonjwa yanayoambukiza.

Lyaniva alitaka wananchi wa wilaya hiyo kuwapa elimu watoto wao kununua vyakula vilivyo katika hali ya usalama ili kujiepusha na magonjwa.

Alisema hali hiyo ya utunzaji mazingira ya makazi yao itasaidia kupunguza hatari katika maeneo yao.

“Kufunika vyakula na kusafisha maeneo kwa kutunza vyoo na mazingira ya kufanyia biashara katika hali ya usafi kutaepusha magonjwa hayo,” alisema Lyaniva.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo