Vijana 250 wajiunga na klabu kupinga ukatili


Dotto Mwaibale

Mussa Mlawa
VIJANA zaidi ya 250 wamejiunga na klabu za kupinga ukatili wa kijinsia katika masoko ya Ilala Boma, Mchikichini na Temeke Sterio, Dar es Salaam.

Mchakato wa kujiunga na klabu hizo ulitokana na mafunzo waliyopata kutoka kwa wawezeshaji sheria wa Shirika la Equality for Growth (EfG) waliyotoa kwa nyakati tofauti katika masoko hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki, Mratibu wa Mradi wa kufungua klabu za mabadiliko katika masoko hayo ambaye pia ni Mwanasheria wa Shirika hilo, Mussa Mlawa, alisema mwitiko wa vijana kujiunga na klabu hizo ni mkubwa mno.

"Hatukutarajia kama mwitiko wa vijana wa kujiunga na klabu hizi ungekuwa mkubwa kiasi hiki," alisema Mlawa.

Alisema changamoto kubwa waliyokuwa nayo ni kwenye soko la Ilala Boma kutokana na ukubwa wake, lakini ndilo liliongoza kwa vijana kujitokeza kwa wingi kuanzia mtu mmoja hadi vikundi.

Alisema mradi huo unafanyika kwa usimamizi wa Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake Tanzania (WLAC) kupitia kampeni ya Tunaweza ambapo EfG wanaiendesha kwenye masoko  matano jijini Dar es Salaam ambayo ni Ilala Boma, Ferry, Mchikichini, Temeke Sterio na Buguruni.

Mlawa alisema vijana hao zaidi ya 250 walijitokeza kujiunga na klabu hizo kutoka masoko ya Temeke Sterio, Mchikichini na Ilala Boma ambapo wataendelea na mchakato huo katika masoko ya Buguruni na Ferry.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo