JPM awahakikishia Wachina ushirikiano


Mwandishi Wetu

Rais John Magufuli
RAIS John Magufuli amewahakikishia ushirikiano wafanyabiashara na wawekezaji wa Shirikisho la Taifa la Utengenezaji Mitambo ya Viwanda la China (CNMIF).

Amesema Serikali yake itawapa ushirikiano wa kutosha katika mpango wao wa kuwekeza kwenye uzalishaji wa nishati ya umeme, viwanda na kilimo nchini.

Rais Magufuli alitoa kauli hiyo jana Ikulu, Dar es Salaam alipokutana na Makamu Mwenyekiti wa CNMIF ambaye ni Mbunge wa Bunge la Wananchi wa China, Zhan Xin.

Alisema Tanzania imejiwekea malengo ya kuongeza uzalishaji umeme kutoka megawati 1,500 na 1,800 zinazozalishwa hivi sasa hadi 10,000.

Rais alisema ili kufikia malengo hayo, wawekezaji wanakaribishwa kuzalisha umeme kwa kutumia vyanzo vilivyopo kama vile gesi, makaa ya mawe na jua.

“Xin kawaambie wawekezaji wenzako wa China waje Tanzania, nchi zetu ni ndugu na marafiki wa miaka mingi, ili kuunga mkono juhudi zetu za kujenga viwanda kwa kuzalisha umeme mwingi na pia kushiriki miradi mingine ikiwamo ya ujenzi wa miundombinu ya reli na barabara,” alisema.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amekutana na Balozi wa Ufaransa nchini, Malika Berak na kuzungumzia utekelezaji wa mambo   ya ushirikiano na miradi ya maendeleo iliyotokana na makubaliano ya mkutano wa wafanyabishara wa Tanzania na Ufaransa, uliofanyika hivi karibuni.

Pia Rais Magufuli alikutana na Kaimu Balozi wa Uturuki nchini, Yunus Belet na Kaimu Balozi wa Jamhuri ya Korea Kusini, Songwon Shin.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo