Z’bar yaaswa kuchangamkia fursa

Suleiman Msuya

Dk Mohamed Shein
WANANCHI wa Zanzibar, wamehimizwa kuchangamkia fursa zilizopo katika Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na kuondokana na dhana kuwa Serikali yao inabaguliwa.

Akiwasilisha mada kuhusu ushiriki wa Zanzibar katika EAC kwenye semina ya masuala ya mtangamano, Ofisa wa Ushirikiano wa Kimataifa kutoka Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Suleiman Haji alitoa ufafanuzi wa kina kuonesha namna Zanzibar inavyoshiriki kwenye EAC.

Haji alieleza kuwa licha ya Zanzibar kuwa sehemu ya Muungano Tanzania, ushiriki wake umedhihirika katika mgawanyo wa miradi ya maendeleo ya EAC, hususan miradi ya miundombinu.

Alisema Zanzibar iliwasilisha mapendekezo ya miradi 10 kwenye Sekretarieti ya EAC na kutokana na vipaumbele vilivyowekwa miradi mitatu imekubaliwa na mchakato wa kuitekeleza unaendelea.

“Mradi wa Bandari ya Marhubi Kisiwani Pemba, upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Pemba na ununuzi wa meli kubwa zitakazosafirisha abiria na mizigo kwenye nchi wanachama wa EAC.

Aidha, alisema Zanzibar inanufaika na miradi inayofadhiliwa na taasisi inayojihusisha na masuala ya kukuza biashara na kupunguza umasikini katika nchi za EAC inayoitwa "East Africa Trademark" (TMEA).

Alisema mradi mwingine unaofadhiliwa na TMEA huko Zanzibar ni ule wa kuwasilisha malamiko kwa njia ya mtandao au ujumbe mfupi wa simu pale inapotokea mfanyabiashara amekumbana na vikwazo visivyo vya forodha katika kusafirisha bidhaa zake ndani ya Jumuiya.

Ofisa huyo alisema Benki ya Dunia (WB), inaendesha mradi wa kutathmini utekelezaji wa Soko la Pamoja kwa upande wa Zanzibar.

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo