Mbunge ataka Serikali igharamie Kidato cha Tano, Sita


Joyce Kasiki, Dodoma

Boniventura Kiswaga
MBUNGE wa Magu Boniventura Kiswaga (CCM) amesema, Serikali  inapaswa kutafakari upya ili wanafunzi wanaochaguliwa kuendelea na kidato cha tano na cha sita wapate elimu hiyo bure .

Kiswaga alitoa kauli hiyo Bungeni jana wakati akiuliza swali la nyongeza ambapo alisema,Vijana wengi wanaochaguliwa kuendelea na masomo hayo ,wanashindwa kuendelea nayo kutokana na kukosa uwezo wa kifedha.

"Hivi sasa tunakabiliwa na uhaba wa wataalam wa sayansi nchini,na hawa wanafunzi wanaochaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano na cha sita wengi wanakuwa wamefaulu masomo ya sayansi na wanakosa uwezo wa kuendelea na masomo hayo kutokana na kushindwa kumudu gharama za masomo,Serikali haioni kwamba inapoteza wataalam,

"Na je,Serikali haioni kwamba ni wakati muafaka kulet bajeti Bungeni ili wanafunzi hawa wasome bure?"

Awali katika  swali la msingi Mbunge hutonalitaka mpango wa Serikali wa kutoa elimu bure kwa wanafunzi we kidato cha tano na cha sita.

Akijibu ,Manyanya alisema,kwa sasa Serikali haina mpango wa kutoa elimu bila malipo kwa wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita .

"Badala  yake imejikita zaidi katika kuboresha miundombinu ambayo ni pamoja na upungufu wa vyumba  vya madarasa ,matundu ya vyoo,majengo ya utawala pamoja na kumalizia changamoto za uhaba wa walimu wa sayansi na vifaa vya kufundishia na kujifunzia ikiwa ni pamoja na masuala ya Tehama.

Mhandisi Manyanya alisema,kukamilika kwa miundombinu hiyo itasaidia kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wenye sifa ya kuingia kidato cha tano wanapata fursa ya kuendelea na masomo yao.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo