Polisi yaamuru baba akamatwe baada ya mtoto kumwibia bastola


Leonce Zimbandu

Simon Sirro
KAMANDA wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Simon Sirro, ametoa amri ya kukamatwa na kufikishwa mahakamani Lazaro Mbise kwa kosa la kuibiwa bastola na mtoto wake Lewis Lazaro ambaye ni mwanafunzi wa chuo Kikuu cha St.Joseph.

Tukio hilo limetokea Mei 4, mwaka huu maeneo ya Mbezi magari saba baada ya Jeshi la polisi kufanikiwa kumkamatwa kijana huo na kukiri baada ya mahojiano.

Kamanda Sirro aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana na kubainisha kuwa mtuhumiwa alikiri kuwa bastola hiyo aliiba nyumbani kwa mzazi wake.

Alisema pia, pamoja na bastola hiyo aliiba Sh. 800,000.

Alisema upelelezi unaendelea ili kujua lengo la mtuhumiwa huyo kuiba silaha hiyo ya baba yake na kufahamu iwapo kama kuna taarifa ya kupotea kwa silaha.

“Huu ni uzembe wa kushindwa kutunza silaha, hivyo mzazi huyo anapaswa kuchukuliwa hatua, ikiwamo kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa kosa hilo,” alisema.

Wakati huo huo Jeshi la Polisi limewakamata watuhumiwa watatu kwa kosa la kuvujisha mtihani wa kidato cha sita somo la kemia katika shule ya sekondari Chang’ombe.

Kamanda Sirro alisema kuwa polisi walipokea siku kutoka kwa afisa wa Baraza la Mitihani Aron Mweteni kuwa Mei 5, mwaka huu katika shule hiyo alimkuta mwalimu Mussa Elius akiingia darasani akiwa na mwanafunzi Ritha Mosha.

Alisema Ritha alikuwa ndiye mtahiniwa wa mtihani wa kidato cha sita unaoendelea akiwa na karatasi ya yenye maswali na majibu ya somo la kemia.

“Baada kufuatilia ilibaini swali hilo ni miongoni mwa mwasawali mtihani huo, hivyo watuhumiwa wote wanaendelea kuhojiwa, akiwamo Mwalimu Innocent Mrutu,” alisema.

Katika hatua nyingine Jeshi hilo limefanikiwa kukamata vipande sita vya meno ya tembo ambavyo thamani yake bado haijafahamika hadi upelelezi utakapokamilika.

Tukio hilo limetokea katika maeneo ya Chanika, Zingiziwa na kufanikiwa watuhumiwa wawili ambao ni Senei Abas mkazi wa Buguruni na Juma Kong’owa fundi ujenzi mkazi wa Gongo la Mboto.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo