Polisi: Mauaji ya Kibiti, Rufiji hayajapoteza amani


Suleiman Msuya

Kamanda Nsato Mssanzya
KAMISHNA wa Mafunzo na Operesheni wa Jeshi la Polisi Tanzania, Nsato Mssanzya, amesema matukio ya uhalifu yanayoendelea maeneo mbalimbali nchini, hasa Kibiti na Rufiji yasitafsiriwe kuwa Taifa limepoteza amani.

Aidha, amesema watu wanaouawa wasihusishwe na vyama vya siasa, kwani hakuna taarifa zinazoonesha kuuawa kutokana na vyama vyao, kwani matukio ya uhalifu yako duniani kote.

Mssanzya aliyezungumza na gazeti hili juzi, alisema Jeshi la Polisi limejipanga kila kona kuhakikisha amani inadumu nchini, akieleza kwamba matukio yanayotokea si taswira sahihi ya kusema Taifa halina amani.

“Kila siku inayopita ni vigumu kutopata taarifa ya matukio ya uhalifu, hivyo hali hiyo isihusishwe na kukosekana kwa amani nchini, lakini pia si vema kuhusisha matukio hayo na siasa,” alisema.

Kamishna alisema hali ya usalama ni nzuri na hakuna mwananchi anayekosa amani.

Alisema wananchi katika maeneo yanayotajwa kuwa na uhalifu wananchi wanajihusisha na shughuli za uzalishaji hali aliyosema inatoa tafsiri ya uwepo wa amani.

Hata hivyo, alisema Jeshi hilo limejipanga kupambana na uhalifu bila kuangalia siasa au vyama, kwani wanaopoteza maisha ni raia wa Tanzania.

Alisema yanayotokea Kibiti na Rufiji ni matukio kama mengine na kinachotakiwa ni wananchi kutoa taarifa za viashiria vya uhalifu na matukio hayo kwa Jeshi hilo, ili liweze kuyafanyia kazi haraka.

Kamishna alisema matukio mengi yanayotokea Kibiti na Rufiji yamekuwa yakitokea vijijini, ambako hakuna polisi tofauti na ilivyo mijini na kwamba kinachohitajika ni taarifa za haraka.

Kamishna aliwataka wananchi kushirikiana na Jeshi hilo kufanikisha kukamata wahusika, ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo