Abiria watakiwa kulinda mizigo yao


Dalila Sharif

DIWANI wa Makangarawe, Temeke, Idd Mahuta, amewataka abiria wanaosimama katika vituo vya mabasi kusubiri usafiri, kuwa makini na mizigo yao ili kuepuka kuporwa na vibaka wa maeneo hayo.

Akizungumza Dar es Salaam jana, alisema abiria huporwa mizigo na simu za mkononi wanaposimama kituoni hapo, huku wengine wakiporwa kupitia madirishani wakiwa kwenye daladala.

“Suala la uporaji limeibuka kwa kasi hasa kwa abiria usiku wanaporudi kutoka kwenye mihangaiko yao ya kila siku. Hali hii si nzuri, kwa sababu hutishia usalama wa wakazi wangu,” alisema Mahuta.

Alisema ni vema wakazi na abiria kuwa makini kuzuia uporaji unaojitokeza na kwamba Polisi Jamii wako pamoja katika kulinda   eneo hilo kwa kushirikiana na polisi wa kata hiyo.

“Kwa sasa kata yetu iko makini na tunamshukuru Mkuu wa Wilaya, Felix Lyaniva kwa kutuongeza askari wanaotembea kulinda usalama wa maeneo hayo nina imani hata matukio ya uporaji yatapungua,” alisema Mahuta.

Aliwataka wakazi kuwa na ushirikiano na kutoa taarifa haraka tatizo linapotokea ili kulifanyia kazi, pia kuhusu suala la usafi aliwashukuru wakazi wake kwa kuwa na umoja katika kutunza mazingira.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo