Uongozi Masaki watakiwa kudhibiti uhalifu


Dalila Sharif

WAKAZI wa Masaki kata ya Toangoma, Temeke, wameuomba uongozi kudhibiti matukio ya uhalifu yanayofanywa na kundi la vijana wanaodhaniwa ni ‘Panya Road’ na kutishia amani, uharibifu wa mali na usalama wao.

Akizungumza Dar es Salaam jana, mmoja wa wakazi hao, Shamira Ramadhani alisema hali si shwari katika eneo hilo, kutokana na kuibuka migogoro ya wananchi wa eneo hilo na vijana wasiojulikana wanaochafua amani ya mtaa huo.

“Takribani wiki ya pili sasa wakazi hatuna usalama katika maeneo yetu kwa kuogopa kuchomewa moto nyumba zetu, kutokana na vitisho vya wahuni hawa,” alisema Shamira.

Jack Haule alisema vijana wanaohisiwa kuwa Panya Rodi hutumia mianya hiyo kuvunja amani pindi mmoja wao anapouawa na wananchi wenye hasira kali baada ya kuiba mali zao.

“Vijana hawa huvamia maeneo huku wakiwa na silaha na kupita kwa makundi maeneo ya Masaki na zipo taarifa za kuchoma moto nyumba mbili kwa petroli na hulipa kisasi cha mwenzao anapouawa,” alisema Haule.

Abdallah Juma alisema Jeshi la Polisi wilayani humo liko pamoja na wakazi hao wakishirikiana kukabiliana na kukamata wahalifu hao.

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo