Changamoto lukuki shule za msingi Kisarawe


Mwandishi Wetu

UHABA wa vyoo, vifaa vya kufundishia na walimu wasio na sifa ni moja ya changamoto inayotajwa kurudisha nyuma jitihada za kuinua sekta ya elimu katika wilaya Kisarawe mkoani Pwani.

Ofisa Elimu Msingi wa Kisarawe, Omari Bane amesema changamoto hizo zimesababisha utoro kwa baadhi ya wanafunzi, hivyo kupunguza idadi ya wanafunzi wanaohudhuria masomo. 

Bane alisema tatizo la vyoo husababisha baadhi ya wanafunzi kuwa watoro kwa sababu baadhi ya wanafunzi huishi mbali na shule.

"Changamoto hizi pia huwakumba walimu waliokosa nyumba za kuishi ambao wanaishi mbali na maeneo ya shule na hivyo hukosa muda wa kuwasadia wanafunzi kwa kukosa muda na kulazimika kuwahi majumbani kwao "alisema Bane

Kuhusu walimu wasio na sifa, alisema ameishukuru Serikali kwa kazi ya kuhakiki vyeti vya watumishi wa umma hasa walimu wa shule za msingi, kwani walimu hao wamekuwa wakichangia kwa kiasi kikubwa kukwama kwa jitihada za kuinua kiwango cha elimu.

Alisema zoezi hilo la kuondosha walimu limeleta pengo kubwa kwa Wilaya na kuongeza kuwa idadi ya uhitaji wao sasa inafikia 80.

Bane alisema  kauli mbiu ya kusoma na kuandika ni msingi wa maendeleo ya Taifa itakwenda sambamba na uhalisia uliopo baada ya kuondoa walimu wasiokuwa na sifa.

Diwani wa Kata ya Kisarawe Abel Mudo alisema  utoaji wa zawadi kwa wanafunzi bora na walimu mara kwa mara  itaongeza chachu na juhudi katika masomo na kuleta msukumo wa ushindani katika taaluma na hivyo kuwafanya wale wavivu waweze kuingia kwenye ushindani na kubadilika.


Mulo alisema ni vyema walimu waliobaki mashuleni kufanya kazi hiyo ya ufundishaji kwa bidii ili kuleta mabadiliko katika sekta ya elimu katika Wilaya na kuinua maendeleo ya elimu na kupunguza umasikini.

Katika sakata la vyeti feki kuna jumla ya watumishi 11 mpaka leo wamekata rufaa kwa kupinga zoezi hilo

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo