Madereva 9 wa wanafunzi kupanda kizimbani


Abraham Ntambara

JESHI la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Kanda Maalumu ya Dar es Saalam kitawafikisha mahakamani madereva tisa waliobainika kuendesha mabasi ya wanafunzi bila leseni stahiki.

Kamishna Msaidizi wa Trafiki wa Kanda hiyo, Awadh Haji alisema jana kuwa tangu waanze operesheni ya kukagua ubora wa mabasi hayo, 185 yalikaguliwa na 119 kubainika na upungufu.

“Hadi Mei 22 tulibaini madereva tisa wakiendesha mabasi bila leseni, hivyo tutawapeleka mahakamani,” alisema Kamishna Haji.

Alisema katika operesheni hiyo, kuna magari yalibainika kuwa na uchakavu wa bodi, hayana mikanda, viti kulegea na matairi mabovu na baadhi ya magari hayo kuwa na ubovu kwenye mifumo.

Aliitaja wilaya ya Kinondoni kuongoza kwa kuwa na magari yasiyofaa kubeba wanafunzi ikifuatiwa na Ilala huku Temeke ikiwa ya mwisho.

Kamishna Haji alisema operesheni hiyo ni endelevu ili kuhakikisha usalama wa wanafunzi.

Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Mohammed Mpinga alisema amewaagiza makamanda wote nchini, kuwasilisha kwake taarifa za ukaguzi wa magari hayo haraka iwezekanavyo.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo