Mitandao ya kijamii yaomboleza vifo vya wanafunzi


*Samia kuongoza watakaoaga miili ya marehemu leo

Suleiman Msuya

WAKATI miili ya wanafunzi 33 wa Shule ya Msingi Lucky Vincent ikitarajiwa kuagwa leo mjini Arusha, makundi mbalimbali ya mitandao ya kijamii ikiwamo WhatsApp yameungana kuomboleza msiba huo kwa kuweka alama ya mishumaa.

Wanafunzi hao, walimu wao wawili na dereva walifariki dunia juzi baada ya basi walilokuwa wakisafiria kuingia kwenye korongo na kupinduka eneo la Rhotia Kata ya Rhotia, Wilaya ya Karatu mkoani Arusha.

Ajali hiyo ilitokea wakati wanafunzi hao wa shule hiyo ya msingi ya mchepuo wa Kiingereza iliyopo jijini Arusha wakielekea kwenye mitihani ya ujirani, kujipima nguvu katika Shule ya Tumaini English Medium.

Katika kile kilichoonesha ni kundi kubwa kuguswa na tukio hilo, wanachama na viongozi wa makundi mbalimbali walipendekeza kuwekwa kwa alama za mishumaa kwenye eneo maalumu la alama ya kila kundi ili kuungana na wazazi na familia zilizopatwa na msiba huo.

Baadhi ya makundi ambayo yalibadilisha alama au nembo zake na kuweka picha ya mshumaa ni Quality Media Group, Wanahabari Tanzania, Maroro na Mikuyuni, Mawazo Huru, Endorsers of Kahangwa, Wasomi wa MNMA, MNMA Great Thinkers na Events & Entertainment.

Mengine ni Sports HQ Tanuey la Fikra, Jukwaa la MNMA, Tasnia ya Mawasiliano, MNH Talks Reloaded, Karagwe Yetu & Friend, Kilimo Kwanza Group, Majirani Goba, Dar Young Africans, WCB, Tukumbukane, United Redblood Fans, Vodacom PL Tanzania, Official WCB Group na Yanga Whatsap Family.

Katika hatua nyingine, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan leo ataongoza wakazi wa Mkoa wa Arusha na mikoa jirani kuaga miili ya wanafunzi 33, wawili wawili na dereva wa Shule ya Lucky Vicent waliopoteza maisha juzi baada ya gari kupata ajali kwenye eneo la Rhotia Kata ya Rhotia, wilayani Karutu.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Arusha, Mrisho Gambo jana ambapo alibainisha kuwa utaratibu wa kuwaaga wapendwa hao utaanza saa mbili asubuhi katika kiwanja cha Sheikh Amri Abeid.

Awali jana mkuu wa wa wilaya alitangaza kuwa marehemu hao wataagwa jana lakini baadae ilitoka taarifa ya mabadiliko ambalo leo wataagwa shughuli ikiongozwa na Makamu wa Rais Suluhu.

Aidha, inatarajiwa katika shughuli hiyo ya kuuga viongozi mbalimbali wa dini, kisiasa, serikali na kijamii watashiriki pamoja na familia kutoa salamu za mwisho.

Marehemu hao walikutwa na ummauti wakati wakiwa safarini Karatu kufanya mtihani wa ujirani mwema na shule ya Msingi Tumaini ambapo walikuwa na msafara wa gari tatu na gari moja ndio ilipata ajali na kusababisha vifo vya watu 36.

Taarifa mbalimbali ambazo zilizopatikana zinadai kuwa gari hiyo ilifeli breki kutokana na mvua inayoendelea kunyesha wilayani hapo.

Vifo hivyo vimeacha simanzi kwa Watanzania wengi huki ikisemekana mmoja wa wazazi ambaye watoto wake watatu wamepoteza maisha alipoteza maisha baada ya tukio hilo.

Kutokana na tukio hilo watu mbalimbali wameendelea kutuma salamu za maombelezo ambapo mmoja wapo ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ambaye aliweka ujumbe unaosema ni watoto wetu, ni wenzetu, hakika ni pigo kubwa sana kwetu, Mungu aziweke roho za marehemu mahali peponi amina.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo