Mahakama yamgomea Lissu


Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imemgomea Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kupewa maelezo ya mlalamikaji ambaye ni Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu kwa sababu imefungwa mikono kisheria.

Uamuzi huo ulifikiwa jana na Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Dk. Yohana Yongolo baada ya kupitia hoja zilizotolewa na pande mbili katika kesi ya uchochezi inayomkabili Lissu.

“Kifungu cha 9 (3) cha CPA kinanifanya nifungwe mikono, kwa sababu upande wa Jamhuri hauwajibiki kuwasilisha maelezo ya mlalamikaji kwa upande wa utetezi.

“Najua mnaitaka taarifa hii kwa sababu inahusu mashtaka yanayomkabili mshtakiwa ambayo yanaangukia katika Sheria ya Magazeti, lakini sheria hiyo iko wazi kabisa kwa sababu tayari upande huo umesema hautamtumia ZCO (mkuu wa upelelezi) kama shahidi,”alisema Hakimu Dk Yongolo.

Pia alisema katika suala ambalo aliliomba wakili wa utetezi, Peter Kibatala la kutaka mkuu huyo aje mahakamani aulizwe maswali lipo chini ya mamlaka yake, kwa hiyo pale atakapoona inafaa atamuita.

“Kwa wakati mwafaka nitakapoona anahitajika nitamuita, lakini hivi sasa siwezi kwa sababu hata sijui mazingira ya kesi yakoje, kwa hiyo nikisema nikubaliane na hilo nitakuwa muongo,”alisema.

Baada ya kusema hivyo hakimu huyo aliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 5, mwaka huu na kuamuru kuwa siku hiyo mashahidi wawepo ili kesi ianze kusikilizwa.

Awali, Kibatala alidai kuwa ni haki ya mshtakiwa kuwa na maelezo ya ZCO kwa sababu yanaweza kutumika kama sehemu ya ushahidi.

Hata hivyo, Wakili wa Serikali Mkuu, Bernard Kongola aliipinga hoja hiyo akidai kuwa kwa mujibu wa sheria hawapaswi kumtumia ZCO kama sehemu ya ushahidi. Anadaiwa alitenda kosa hilo kinyume cha kifungu namba 32 (1)(b) cha Sheria ya Magazeti iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo