Dau ateuliwa kuwa balozi Malaysia


RAIS John Magufuli amem­wapisha aliyekuwa Mkuru­genzi Mkuu wa Shirika la Hi­fadhi ya Jamii (NSSF), baada ya kuteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malaysia.

Kwa mujibu wa taarifa iliyo­tumwa jana kwa vyombo vya habari kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, uapishaji huo ulifanyika jana.

Taarifa hiyo ilisema Balozi Dk Dau (pichani) anajaza na­fasi iliyoachwa wazi na ali­yekuwa Balozi Dk Aziz Mlima ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Af­rika Mashariki na Kikanda.

Wakati huo huo, Rais Magu­fuli aliwaapisha makatibu tawala wa mikoa mitatu alio­wateua mwishoni mwa wiki iliyopita.

Walioapishwa ni Eliya Ntandu anayekuwa Katibu Ta­wala wa wa Mkoa wa Songwe ulioanzishwa rasmi Februari, Adoh Mapunda anayekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara.

Mapunda anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Benedict ole Kuyan ambaye amestaafu, Tixon Nzunda anakuwa Kati­bu Tawala wa Mkoa wa Rukwa kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Symthies Pangisa am­baye amestaafu.

Baada ya kuapishwa, Balozi Dau na makatibu tawala hao watatu walikula kiapo cha ahadi ya uadilifu kwa viongo­zi wa umma kilichoongozwa na Kamishna wa Maadili, Jaji mstaafu Salome Kaganda na kushuhudiwa na Rais Magu­fuli.

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo