Mahakama Kuu yatupa maombi ya wakili BoT


Grace Gurisha

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, imetupilia mbali maombi ya Wakili wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Kharimu Rashidi ya kutaka waandishi wa habari wasiandike kesi inayomtaka Gavana, Profesa Benno Ndulu kwenda mahakamani kueleza ni jinsi gani watakavyotekeleza amri kulipa sh. bilioni 92.

Amri hiyo ilitolewa na Msajili wa Mahakama hiyo, Project Kahyoza ya kuitaka BoT iilipe Coast Textiles Ltd fedha hizo na kama watashindwa kufanya hivyo, watafungwa jela kama wafungwa wa kesi ya madai.

Ombi hilo liliwasilishwa jana mbele ya Jaji Ama Munisi wa mahakama hiyo, ambapo Wakili Rashid alidai kuwa anaona watu wanaandika wakati katika utambulisho wao hawakujitambulisha na pia hilo linasikilizwa chemba, kwa hiyo hapaswi mtu mwingine kusikiliza.

Hata hivyo, Jaji Munisi alitofautiana na wakili huyo na kutupilia mbali hoja yake, kwa kusema kuwa kesi hiyo kweli inasikilizwa chemba, lakini ni suala ambalo liko wazi. “Hatusikilizi suala hili kwa faragha, ndiyo tunasikiliza kwenye chumba kidogo, lakini ni suala ambalo liko wazi kwa hiyo kama watu wanaandika waache waandike,”alisema Jaji Munisi.

Kesi hiyo ilikuja jana kwa ajili ya kusikiliza pingamizi la Coast Textiles Ltd, ambapo waliomba mahakama hiyo kutupilia mbali maombi ya Gavana na Mafuru ya kutaka kuzuia utekelezaji wa amri kutakiwa kulipa sh.bilioni 92, lakini ilishindikana kwa sababu benki hiyo iliwasilisha maombi.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo