Chadema kutoa msimamo wa Ukuta leo


Fidelis Butahe

MWEZI mmoja baada ya Chadema kusitisha Operesheni Ukuta kupinga inachokiita ukiukwaji wa haki za binadamu na ukandamizaji wa demokrasia, leo inatarajia kutoa mwelekeo wa mkakati huo.

Operesheni hiyo ilipangwa kuzinduliwa Septemba mosi nchini kwa maandamano na mikutano ya hadhara kama maazimio ya Kamati Kuu ya Chadema, baada ya chama hicho kukumbwa na vikwazo kadhaa kuendesha shughuli zake, ikiwa ni pamoja na kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara.

Siku moja kabla ya kufanyika kwa operesheni hiyo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alitangaza kuisitisha kwa mwezi hadi kesho, ili kutoa fursa kwa viongozi wa dini kusemezana na Rais John Magufuli na Serikali yake.

Akizungumza na JAMBO LEO jana, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema: “Kuhusu Ukuta, kesho (leo) tutatoa msimamo wetu juu ya kitu
tutakachofanya.”

Alisema operesheni hiyo ilisitishwa kutokana na sababu za msingi zilizoelezwa, hivyo kauli ya chama hicho leo itafafanua kwa kina kuhusu mambo yote yaliyojitokeza katika kipindi hicho cha mwezi.

Wakati Lissu akieleza hayo, hadi jana hakukuwa na taarifa zozote za kufanyika kwa kikao kati ya viongozi wa dini na Serikali.

Viongozi hao waliitaka Serikali na Chadema kufikiria amani ya nchi na kutafuta njia mwafaka za kumaliza msuguano wa kisiasa hasa baada ya chama hicho kushikilia msimamo wake wa kufanya mikutano na maandamano.

Wakati Chadema wakijipanga kutoa tamko lao, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda jana alisisitiza kuwa Oktoba mosi ni Siku ya Kupanda Miti jijini humo ambapo viongozi mbalimbali watahudhuria.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo