Darasa la saba kuanza mitihani leo



BARAZA la Mitihani la Tanzania (Necta), limetangaza kuanza kwa Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE), utakaofanyika leo na kesho nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde alisema jumla ya watahiniwa waliosajiliwa kufanya mtihani huo ni 795,761 tofauti na mwaka jana ambapo walikuwa 775,729 .

Alisema kati ya wanafunzi hao wavulana ni 372,883 sawa na asilimia 46.86 na wasichana ni 422,878 sawa na asilimia 53.14 watakaofanya mitihani kwenye shule 16,350.

“Kati ya watahiniwa wote waliosajiliwa, watahiniwa 765,097 watafanya mitihani yao kwa Kiswahili na wengine 30,664 watatumia Kiingereza ambacho wamekuwa wakikitumia kujifunzia,’’ alisema Dk Msonde

Alisema watahiniwa wasioona waliosajiliwa kufanya mitihani ni 95 wakiwamo wavulana 57 na wasichana 38, wenye uono hafifu ambao huhitaji maandishi makubwa ni 810 kati yao wavulana ni 402 na wasichana ni 408.

Alisema masomo yatakayofanyiwa mitihani ni Kiingereza, Kiswahili, Hesabu, Sayansi, Maarifa ya Jamii ambapo somo la Tehama halitafanyiwa mitihani kwa sababu ni shule chache tu zilizokuwa zinafundishwa bila vifaa vya kutosha.

Alisema maandalizi ya mitihani yamekamilika ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa karatasi, fomu maalumu za OMR za kujibia na nyaraka zote muhimu zinazohusu mitihani katika halmashauri zote nchini.

Dk Msonde, alitoa mwito kwa walimu na wanafunzi kuwa waaminifu kwenye mitihani huku akizitaka jamii zinazozunguka maeneo ya shule kuwa tulivu katika kipindi ambacho wanafunzi watakuwa wanafanya mitihani yao.

“Tunatoa mwito kwa wasimamizi kufanya kazi yao ya usimamizi kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu,B araza halitasita kuchukua hatua kwa mtu atakayehusika na udanganyifu wa mitihani,’’alisema Dk Msonde.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo