Mbunge: Waziri wa Fedha ajiuzulu


Mwandishi Wetu

Waziri Mpango
MBUNGE wa Tunduma, Frank Mwakajoka (Chadema), amewataka wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuacha usanii katika masuala ya Kitaifa akisema wanachofanya wanaumiza wananachi hasa wa vijijini.

Mwakajoka amesema iwapo Taifa lingekuwa linaendeshwa kwa misingi ya uadilifu na uwajibikaji Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango angeapaswa kujiuzulu.

Alisema pamoja na Serikali kushindwa kutekeleza Bajeti zilizotengwa katika maendeleo takribani miaka, yote bado wabunge wa CCM wamekuwa wakiunga mkono na kupongeza.

Alisema katika Bajeti ya 2016/17 zaidi ya Sh. trilioni 11 fedha zilizoenda katika miradi ni Sh. trilioni 4 sawa na asilimia 38 jambo ambalo linaashiria kuwa utekelezaji ni tatizo.

“Hapa bungeni tulitenga Bajeti ya maendeleo katika kilimo sh. bilioni 101 fedha zilizoenda ni Sh. bilioni 3, umwagiliaji ilitengwa Sh. bilioni 35 ila imeenda Sh. bilioni 1 jambo ambalo liaashiria kuwa hakuna nia ya kutatua changamoto za nchi,” alisema.

Alisema mwaka 2015/16 wakati wa Serikali Rais mstaafu Jakaya Kikwete alitenga zaidi ya Sh. bilioni 88 kwa ajili ya pembejeo za kilimo ila leo wametenga Sh. bilioni 10 halafu wanapongeza Serikali.

Alisema ni jambo la kusikitisha kuona serikali inakimbilia kutoa mabilioni ya fedha kununua ndege wakati hali ya afya ni mbaya nchini.

Mwakajoka alisema Watanzania hawajawahi kusema wanahitaji ndege na reli hivyo Serikali ingepaswa kujikita katika sekta ambazo zinasaidia jamii kubwa kama kilimo.

Alisema uwekezaji ukielekezwa katika kilimo, mifugo na uvuvi ni kundi kubwa ambalo litafaidika kwa haraka hivyo dhana ya uchumi wa viwanda itaanza kutimia kwa haraka.

“Napenda kusema katika kipindi hiki tunapaswa kuwekeza kwa wafugaji, wavuvi na wakulima kwani takwimu zinaonesha kuwa kundi hilo ni asilimia 75 ya Watanzania,” alisema.

Alisema ufinyu wa Bajeti katika sekta ya viwanda itakwamisha mpango wa kuleta viwanda hivyo kuwataka wabunge waachane na utamaduni wa kusema ndio kwa kila jambo.

Akizungumzia hoja ya kumtaka Waziri Mpango kuwajibika kwa kile alichodai kuwa ameshindwa kusimamia wizara alisema wakati wananchi wakitambua kuwa wana mchumi ameanza kuingiza wamachinga kulipa kodi.

Alisema waziri angepaswa kuja na hoja yenye tija kwa nchi na wananchi na kuwa kuwahusisha wamachinga katika kodi ni kupoteza mwelekeo.

“Katika dunia hii ulishaona wapi wamachinga wakilipa kodi mabya zaidi hamjaweka mazingira rafiki ya watu hao kufanya biashara wakiwa huru,” alisema.

Aidha, Mbunge huyo ametoa angalizo kwa Serikali kutaka kumchunguza na kuwashtaki waliokuwa wanasheria wakuu katika suala la mchanga wa madini (makinikia), kwa kile alichodai kuwa hakuna ambaye atabakia salama.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo