‘Maendeleo Dar yatatokana na wakazi wake’


Suleiman Msuya

Jiji la Dar es Salaam
MEYA wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita amewaasa wananchi wa jiji hilo kudumisha amani, mshikamano, upendo na ushirikiano ili kuweza kufanikisha mipango mbalimbali waliojiwekea.

Mwita aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na wananchi waliowaalika katika hafla ya futari iliyofanyika viwanja vya Ofisi ya Meya vilivyopo kwenye Ukumbi wa Karimjee.

Alisema amani inayoonekana kuwepo kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan inapaswa kuwa endelevu ili kuchochea ujenzi wa jiji hilo.

Meya alisema iwapo jamii ya Dar es Salaam itazingatia amani, mshikamano, upendo na ushirikiano ni dhahiri kuwa mipango mbalimbali waliyojiwekea itafanikiwa.

“Tunahitaji maendeleo katika sekta mbalimbali njia sahihi ya kufikia huko tunapaswa kuwa na amani, umoja, mshikamona, ushirikiano na upendo hivyo naamini kupitia Ramadhan na futari hii tutakuwa na mwanzo mzuri,” alisema.

Aidha, alitumia futari hiyo kuwataka viongozi mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam kujikita katika kutoa huduma za kijamii ili kuwatatulia wananchi changamoto zinazowakabili.

Meya Mwita alisema iwapo kila kiongozi atasimamia majukumu yake ipasavyo itakuwa rahisi kwa Serikali kufikia malengo ya kuboresha huduma za kijamii.

Aliwataka wananchi kuitumia ofisi yake ili kuweza kutatua changamoto zinazowakabili na wasisubiri mpaka hali iwe mbaya ndio wamtafute.

“Napenda kutumia nafasi hii kuwaomba wananchi wa Dar es Salaam kutumia ofisi ya jiji ipasavyo kwani ipo kwa ajili yenu mimi nipo tayari kuwasikiliza,” alisema.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo