Celina Mathew
SERIKALI
ya Uganda imeamua kutumia usafiri wa maji kusafirisha bidhaa na huduma zake
kutokana na unafuu kuliko njia ya reli inayoonekana kuwa aghali zaidi.
Katika
uamuzi huo, Uganda imechagua bandari ya Dar es Salaam kuwa sehemu yake ya
kusafirishia bidhaa na huduma kwa kuwa ni nafuu na salama zaidi kuliko bandari zingine.
Hatua
hiyo inakuja wakati nchi hizo mbili zikitarajiwa kunufaika na bomba la mafuta
kutoka Uganda hadi Tanga ambapo ushirikiano huo umeendelea kuleta manufaa kwa mawaziri
wa sekta ya usafirishaji kuendelea na mazungumzo ya kuendeleza ukanda wa kati wa
usafirishaji na uchumi endelevu.
Akizungumza
Dar es Salaam jana wakati kusaini makubaliano katika usafirishaji kati ya nchi
hizo mbili, Waziri wa Usafirishaji wa Uganda Henry Bagiire alisema Serikali
yake inatamani kuboresha ukanda wa kati kama mkakati wa kuhakikisha wanafikia
uchumi wa kati.
Alitaja
maeneo ambayo yanahitaji utekelezaji kuwa ni pamoja na kuboresha kivuko cha mv
Kaawa, kuandaa bandari za Bell na Jinja na kuifanyia matengenezo bandari ya
Bukasa.
“Usafiri
wa maji ndio chanzo kikuu cha kusafirisha bidhaa kirahisi, hivyo uchumi wa nchi
yetu hautafanikiwa bila njia hiyo, hata ukingalia nchini ukitaka kusafirisha chai
kwa reli unatumia dola milioni 120 kwa tani tena kwa ufanisi lakini kwa maji ni
dola milioni 60,” alisema.
Alisema
ukitumika usafiri wa maji kwa kiasi kikubwa utaokoa dola milioni 40 kwa mwaka
na kwamba kwa mwaka 2003 ukanda huo ulihudumia tani 330,000 sawa na asilimia
30.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa alisema kufanikiwa
kwa njia hiyo ya Uganda kusafirisha bidhaa zake kupitia bandari ya nchini kutaleta
ufanisi kwenye sekta hiyo.
“Uganda
ni rafiki zetu, hivyo tunashirikiana nao kuhakikisha wanatumia bandari hii kwa
kuwa itasafirisha mizigo kwa ufanisi kutoka Dar es Salaam-Mwanza hadi Kampala,
kwa saa 24 tu,”alisema.
Alisema
suala hilo likisimamiwa vizuri, mizigo ya nchi hiyo itafikishwa kirahisi na kwa
muda mfupi na kuondoa urasimu wa wateja kupewa risiti nyingi na badala yake watapewa
moja tu ya gharama zote.
Aliongeza
kuwa pia utaleta faida kwa pande zote mbili, kwa kuwa ni wajibu kwa nchi hizo
kutumia bandari za pande zote kwa kuwa ni ndugu kwenye masuala ya biashara.
Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Deusdedit Kakoko alisema kufanikiwa
kwa makubaliano hayo, kutawezesha mizigo ya Uganda kusafirishwa kwa siku siku
nne badala ya tano kupitia njia ya Mutukula.
0 comments:
Post a Comment