Kampuni mmiliki wa Star TV hatarini


Mwandishi Wetu, Mwanza

OFISI za Kampuni ya Sahara Media Group (SMG) inayomiliki kituo cha televisheni cha Star, Radio Free Africa na Kiss Fm zimefungwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa deni la Sh bilioni 4.5, hivyo kuwa hatarini kupigwa mnada kufidia deni hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kusitisha shughuli za kampuni hiyo kwa kutia kufuli milango yake jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Udalali ya Sukar, Lyasuka Salehe ambayo ni mawakala wa TRA, alisema walitoa siku 14 kwa mmiliki wa kampuni hiyo, Anthony Diallo kulipa deni hilo.

"Hizi siku 14 tulizotoa akishindwa kulipa tutaitisha mnada wa hadhara kukomboa kodi ya Serikali," alisema Salehe.

Meneja wa TRA wa Mkoa wa Mwanza, Ernest Dunde alisema kazi ya Serikali ni kukusanya kodi, yeyote anayedaiwa lazima alipe hivyo ukusanyaji madeni ni endelevu na yeyote anayedaiwa lazima alipe.

Meneja wa Utumishi na Utawala wa Kampuni hiyo,  Raphael Shilatu alisema ni kweli wamekuwa na malimbikizo ya kodi ya muda mrefu, huku akitaja sababu kuwa ni Serikali kuwataka kutoka analojia kwenda dijitali.

"Hali hiyo ilitufanya kuyumba sana kiuchumi baada ya kufanya  uwekezeji mkubwa hivyo kujikuta tumeyumba kiuchumi na kukaribisha madeni yaliyosababisha hali kama hii," alisema

Shilatu pia aliwataka wapenzi na wasikilizaji wa vyombo hivyo kuwa na moyo wa uvumilivu na kuongeza kuwa kipindi hiki ni cha mpito na mambo yatakuwa sawa.

Kabla ya kufunga milango, wafanyakazi walionekama kupigwa  butwaa huku wengi wao wakitoa magari yao yasifungiwe ndani.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo