'Upinzani wajipanga kuwa chama kimoja'

Celina Mathew

MWENYEKITI wa Chama Cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia amesema mazungumzo ya mpango wa kuunda chama kimoja cha siasa cha upnzani nchini yanaendelea na kwamba mkakati huo unafanyika kwa vitendo bila maneno.

Hata hivyo, Mbatia mabaye pia ni mwenyekiti mwenza wa Umoja wa Vyama Vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), amekiri kuwa changamoto iliyopo katika kuunda chama hicho ni suala la uaminifu aliosema inabidi uwepo baina yao kabla ya mchakato huo kufanyika.

Mbatia alitoa kauli hiyo jana wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Funguka kupitia Kituo cha Televisheni cha Azam Two kinachoendeshwa na mtangazaji mahiri Tido Mhando.

"Mazungumzo ya kuwa na chama kimoja yanaendelea kwa vitendo bila maneno maana mtihani wa kwanza ni bungeni kuwa kitu kimoja, lazima tuwe kitu kimoja, "alisema.

Alisema kila chama cha siasa kimesajiliwa na ndio maana kinaendesha majukumu yake kama kawaida na yakiwepo mambo ya pamoja lakini hukutana kujadilikwa pamoja ili kupata mwafaka ya yanayowahusu na kuwaunganisha.

Mbatia alisema wanaovihukumu vyama vya upinzani kwa kutokuwa na umoja kwa sasa hawawatendei haki akisema ni mapema na kusisitiza kwamba mchakato huo wa kuunda chama hicho unaendelea.

"Kutuhukumu ndani ya miezi minane tuu baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu, kutuhukumu namna hii mnakuwa hamtutendei haki hata kidogo,"alisema.

Alisema zipo kanuni bungeni na maandishi mbalimbali ndani ya ukawa kupitia kamati kuu ya Ukawa , kamati ya makatibu wakuu , na kamati ya ukawa ambayo huwa wanakaa pamoja kuzungumza mambo yanayohusu umoja huo kwa utaratibu.

Alisema suala la kuaminiana ni jambo la msingi ndani ya umoja huo kwani kuujenga kunahitaji utashi zaidi wakizingatia umuhimu wake na tija kwa Taifa.

"Mimi kukuamini wewe na wewe kuniamini mimi kwa mfano Mwalimu Julias Nyerere mwaka 1962 alikaa na Karume alikuwa na utashi wa kukaa pamoja ii kujadili namna ya kuunganisha Zanzibar wawe kitu kimoja," alisema.

Alisema suala hilo lilikuwa tendo la maridhiano kati ya pande mbili na kwamba ndio sababu lilifanikiwa kutokana na kuwepo kwa kuaminiana na baada ya siku mbili suala hilo lilifanyika na nchi ikapata Muungano.

Aliongeza kwa hata muafaka wa Zanzibar ulianza kati ya Mzee Amani Karume na aliyekuwa Rais kipindi hicho na Maalim Seif Sharrif Hamad, hivyo umainifu wa viongozi hao n kuaminiana kwao inaleta viongozi.

Mbatia alisema wakati wanaanzisha ukawa lengo lao lilikuwa ni kuwa na umainifu na kwamba mazungumzo yalikuwepo ambapo walifanya mtihani huo mwaka jana na kufanikiwa kumteua mgombea mmoja kupitia umoja huo

Alisema japo kuna sehemu nyingine kwenye majimbo waliyogawana kuliibua fikra na mijadala tofauti.

Mbatia alisema uwezo wa kuunda chama kimoja upo pale pale na waanamini kuwa watashinda.

Ukawa kunufaisha Chadema

Mbatia alionekana kukwepa swali kuhusu Ukawa kufaidisha Chadema, badala yake alisema kuwa NCCR 'unaweza kuwa na fikra hizo lakini nilisema mwanzoni kuwa hekima ni ule uwezo anaopewa mwanadamu wa kufanya maamuzi yenye busara kwa kutumia uzoefu pamoja na taarifa sahihi'.

Alisema si kwamba chama kinachotoa mgombea urais ndiyo kinapata maslahi zaidi kuliko kingine, bali kinachoangaliwa ni maslahi na kukuza utu wa Watanzania.

Alisema shabaha yao kubwa si kupambana na CCM pekee bali kuona ustawi wa Tanzania, watu wake wakiwa na elimu shirikishi, bora na kwa wote.

Alipoulizwa kama hana wasiwasi kwamba chama chake kitadhoofika  katika Ukawa Mbatia alisema: “Ninaamini changamoto tulizonazo ndani ya chama changu na migogoro ya kifikra inatuimrisha tuzidi kuipotezea.”

Alisema ingawa watu wanaweza kuona kama NCCR imedhohofika lakini ni msaada kwa Ukawa ili kuwaunganisha wapinzani pamoja.

Akwepa kuzungumzia Ukuta

Kiongozi huyo pia alipotakiwa kueleza kama  anaunga mkono Operesheni ya Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta), alisema yeye si msemaji mkuu wa Chadema .

Alisema kwakuwa Chadema ni washirika ndani ya Ukawa na wanachozungumzia ndani ya Ukuta ni kupinga uonevu ni kutaka taratibu zifuatwe hususani katiba inayopingwa kwa sasa iweze kutekelzwa ibara ya 20.

Alifafanua kuwa Ibara hiyo inazungumzia haki ya watu kujumuika, kuzungumza kuweza kushiriki katika uhuru wa kauli.

Mbatia alisema kuwa inahitajika meza ya maridhiano ili changamoto zilizopo nchini zimalizike.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo