Lipumba yametimia CUF, Sakaya, Maftah waweka rehani ubunge


Suleiman Msuya

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amesimamishwa uanachama wa chama hicho huku Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho(Bara), Magdalena Sakaya akivuliwa nyadhifa zake zote na kusimamishwa uanachama.

CUF pia imemsimamisha uanachama Mbunge wa Mtwara Mjini, Maftah Nachuma hatua ambayo inaweka rehani ubunge wake na Sakaya ambaye pia ni mbunge wa Kaliua mkoani Tabora.

Aidha, CUF imemfukuza uanachama Katibu wake wa Baraza la Wazee, Shashi Lugeye huku pia ikiwasimamisha uanachama, Thomas Malima na Naibu Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano, Abduli Kambaya.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili wakati linakwenda mitamboni kutoka ndani ya kikao cha Baraza Kuu la CUF mjini Zanzibar, zinaeleza kwamba uamuzi wa kumfukuza Shashi umefuatia kupewa nafasi ya kujieleza, huku Lipumba, Sakaya na wengine wakishindwa kuhudhuria mkutano huo.

Taarifa zinasema Baraza Kuu limewaadhibu wanachama 15, ambapo nafasi ya Sakaya sasa itakaimiwa na Joram Nachingwa, huku ile ya Kambaya ikikaimiwa na

Mbarak Maharagande.

Kwa mujibu wa Katiba ya CUF, wanachama hao waliosimamishwa na kufukuzwa hawana nafasi nyingine ya kukata rufaa.

Wiki iliyopita baada ya Mkutano Mkuu Maalum wa CUF uliovunjika jijini Dar es Salaam, Jambo Leo lilimnukuu Sakaya ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kaliua, akisema yupo tayari kwa uamuzi wowote utakaochukuliwa kuhusu yeye kwani anaamini  kwamba anasimamia Katiba na si maslahi binafsi.

Aliyasema hayo alipoulizwa kuhusu kuwepo kwa taarifa kuwa Baraza Kuu la CUF, linatarajia kukutana wakati wowote ili kumjadili Profesa Ibrahim Lipumba na baadhi ya wanachama akiwemo yeye.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo