Milioni 23 kupata vitambulisho


Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dk. Modestus Kipilimba

Na Lilian Lundo wa MAELEZO

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imeeleza kuwa ifikapo Desemba 31 Watanzania milioni 23 watakuwa na namba za utambulisho wa vitambulisho vya uraia. Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Mamlaka hiyo, Rose Mdami alisema jana kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo Rais John Magufuli kwa NIDA kuweka saini ya mwombaji na mtoa vitambulisho.

"Tulianza kutekeleza agizo la Rais tangu Juni, inamaanisha vitambulisho vyote tulivyochapisha kuanzia Juni vina sainihizo mbili na tarehe ya kuzaliwa mwombaji," alifafanua Mdami.

Alieleza kuwa ugawaji wa vitambulisho hivyo unasubiri uzinduzi wa Rais Magufuli atakayekabidhiwa kitambulisho namba moja na baadaye vitagawiwa kwa wengine. Alisema ili mwananchi apate kitambulisho cha uraia, lazima afike ofisi za NIDA akiwa na vielelezo vinavyoonesha mwaka wa kuzaliwa uthibitisho wa uraia hii ni kutokana na NEC kutokuwa na viambatanisho hivyo.

Alibainisha kuwa mwananchi mwenye namba ya utambulisho anaweza kupata huduma zote kutokana na namba hiyo kutobadilika na kutumika hata baada ya kitambulisho kuchapishwa.

Alisema mpaka sasa Watanzania milioni 2.7 wamepewa vitambulisho††hivyo na milioni 6.5 wamesajiliwa kwa ajili ya kupewa. Aidha, vitambulisho vya zamani vitaendelea kutumika mpaka utakapotangazwa utaratibu wa kuvibadilisha na kupata vipya.

Alitoa ufafanuzi juu ya malalamiko ya baadhi ya watu kwamba kuna mlolongo mrefu wa kupata vitambulisho hivyo kwa kuwa NIDA haina namna ya kufupisha mlolongo huo, kwani kufanya hivyo ni sawa na kuuza uraia wa Tanzania.

Alisisitiza kuwa lazima NIDA ijiridhishe na uhalali na sifa za mwombaji kwa kupitia vielelezo vinavyohitajika.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo