Utupaji wa chakula nchini Marekani


Na William Shao

Chakumb,a klsd lashds dash djkhsad askdgsa dgjksadsajk
Baraza la Kuhifadhi Mali za Asili la Marekani linasema kwamba asilimia 40 hivi ya chakula chote nchini humo hakitumiwi. Kwa mfano, inakadiriwa kwamba asilimia 7 ya mazao yote hayavunwi, kwamba asilimia 17 ya vyakula vya mikahawani haviliwi, na kwamba familia hutupa asilimia 25 hivi ya vyakula wanavyonunua.

“Taifa letu linapaswa kujifunza mambo mengi ambayo kwa sasa yanatendeka barani Ulaya," likasema jarida 'European Parliament News' la January 19, 2012. Uingereza na Jumuiya ya Ulaya wamefanya utafiti ili kuelewa kinachosababisha tatizo hili.

Januari 2012, kwa mujibu wa jarida 'European Parliament News', Bunge la Ulaya lilipitisha azimio la kupunguza taka za vyakula kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2020 na kuutaja mwaka 2014 kama "Mwaka wa Ulaya Dhidi ya Taka za Vyakula". Mwaka huo, 2014, Uingereza ilifanya kampeni iliyojulikana kama "Penda Chakula, Chukia Taka."

Kwa mujibu wa Idara ya Kilimo ya Marekani (USDA), kaya pamoja na wafanyabiashara wa chakula kama mahoteli na migahawa, kwa pamoja ziliharibu chakula cha thamani ya zaidi ya paundi bilioni 86 za Uingereza (sawa na Tsh. 245,775,740,000,000) kwa mwaka 2008 pekee, au asilimia 19 ya chakula chote kilichosambazwa nchini Marekani kwa mwaka huo. Hiyo ni kwa mujibu wa jarida ‘The Journal of Consumer Affairs’ chini ya makala “The Value of Retail- and Consumer-Level Fruit and
Vegetable Losses in the United States.

“Asilimia 40 ya chakula chote kinachonunuliwa kwa ajili ya hoteli na migahawa kinatupwa kabla hakijamfikia mlaji,” linasema jarida USDA Food Review la Marekani na kuongeza kuwa kiasi kingine cha chakula “…kinahifadhiwa lakini hakiliwi…” hadi kinakuwa taka.

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo