Kumsifu mtoto kupita kiasi tatizo


Watoto wadogo watoto wadogo watoto wadogo
Watafiti wamegundua kuwa kuwasifu watoto kupita kiasi ni “mwelekeo usiofaa”. Kwa mujibu wa jarida Psychology Today, vijana wengi wanapoanza kufanya kazi wanakuwa na mtazamo wa kudai vitu kwa nguvu—mtazamo huo unawafanya wadai mafanikio hata ikiwa hawajafanya chochote kustahili mafanikio hayo.

Baadhi yao hudhani kwamba watapandishwa cheo haraka, hata kabla ya kuwa stadi katika kazi yao. Wengine wanajiona kuwa bora na kwamba wanastahili kutendewa hivyo—wasipotendewa hivyo, “…wanahuzunika na hata kufanya ‘mgomo’ baridi”.

Lakini ni nini kinachosababisha yote hayo? “Nyakati nyingine huenda mtazamo wa kudai vitu kwa nguvu ukatokana na malezi ya mtu,” linaandika jarida hilo na kuongeza, “Kwa mfano, wazazi fulani wameathiriwa sana na wazo ambalo limeendelezwa katika miaka ya karibuni kwamba kujiheshimu ndilo jambo muhimu zaidi na linapaswa kuzingatiwa.” Ilisemekana kwamba wazo hilo linafaa kwa kuwa “…ikiwa mtoto anafaidika anaposifiwa kidogo, basi akisifiwa sana atafaidika zaidi”.

Kwa upande mwingine, ilisemekana kwamba kumwonyesha mtoto kwamba hufurahishwi na mambo anayofanya kutamvunja moyo. Na mzazi aliyefanya hivyo alionekana kuwa mzazi asiyefaa kwani ulimwengu ulikuwa na lengo la kuwafanya watu wajiheshimu. Wazazi waliambiwa kwamba hawapaswi kumfanya mtoto ahisi kuwa amekosea.

Kwa sababu hiyo, wazazi wengi walianza kuwasifu sana watoto wao hata wakati ambapo hawakufanya jambo lolote linalostahili sifa. Mtoto alipotimiza jambo lolote, hata liwe dogo kiasi gani, alisifiwa; alipofanya makosa, hata yawe makubwa kiasi gani, yalipuuzwa.

Wazazi waliamini kwamba siri ya kumfanya mtoto ajiheshimu ni kupuuza makosa na kusifu jambo linguine lolote. Kuwafanya watoto wajihisi vizuri kukawa jambo muhimu zaidi kuliko kuwafundisha kujitahidi kutimiza mambo ambayo yatawafanya wajihisi vizuri.

Wanasaikolojia wanaelekeza kwamba usiwasifu watoto kwa sababu tu unataka kuwafanya wajihisi vizuri. Huenda hawatafaidika.

Kitabu Generation Me © cha Jean M. Twenge kinasema: “Mtu hujiheshimu kikweli kwa sababu ya kuboresha vipawa vyake na kujifunza mambo, hajiheshimu kwa sababu tu ya kusifiwa bila sababu.”


Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo