Mbaroni akidaiwa kughushi nyaraka

Edith Msuya

IDARA ya Habari, Maelezo imemkabidhi kwa Jeshi la Polisi mkazi wa Dar es Salaam Joseph Sheka, anayemiliki kampuni ya Fukanu kwa tuhuma za kuwasilisha nyaraka za kughushi kwa nia ya kuitapeli Serikali ili kusajili gazeti.

Tukio hilo ambalo lilitokea jana saa saba mchana lilishuhudiwa gari ya Jeshi la Polisi likifika idarani hapo na kuwakamata watu wawili, mmoja akiwa ndiye Sheka ambaye alitarajiwa kuwa Mhariri wa Gazeti hilo.

Akizungumza jana Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Idara hiyo, Dk Hassan Abbas ambaye hakuweka wazi walitumia njia gani ili kuwakamata, alisema mtuhumiwa huyo alifikisha nyaraka hizo idarani hapo akitaka kusajili gazeti liitwalo Lete Mambo.

Alisema mtuhumiwa huyo anashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa mahojiano zaidi ili kubaini ukweli wa tukio hilo.

"Anatuhumiwa kuwasilisha nyaraka mbalimbali akidai kuwa ni za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambapo uchunguzi wa awali ulibaini kuwa alighushi mihuri na saini za maofisa wa Mamlaka hiyo, ili kufanikisha azma yake," alisema.

Aidha, alisema taasisi za kiserikali huwa makini katika kipindi kama hiki kwa matukio hayo yanayoonekana kuwa makubwa.

Hata hivyo, aliiasa jamii kuwa huu si wakati wa kujaribu kuishi kwa njia zisizo halali na badala yake kufuata taratibu halali mtu anapotaka huduma katika maeneo mbalimbali ya ofisi za umma.

"Bila kuathiri uchunguzi unaondelea na utakaotolewa taarifa zaidi na Polisi naomba nitoe rai kwa ofisi za umma kuwa makini na nyaraka zinazowasilishwa kwao, kwani zingine ni kwa ajili ya kuitia hasara Serikali,” alisema Dk Abbas.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo