Polisi wagomea Operesheni Kata Funua ya Chadema


Suleiman Msuya

WAKATI Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Festo Kiswaga, akitangaza kukataza chama cha Chadema, kuzindua Oporesheni Kata Funua iliyopangwa kuzinduliwa leo, Kamanda wa Polisi mkoa huo, Onesmo Lyanga, amepata kigugumizi kuzungumzia operesheni hiyo na kumtupia mpira mkuu wa mkoa huo huku chama hicho kikisisitiza kuuzindua leo.

Jana Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Festo Kiswaga, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Bariadi alikaririwa na vyombo vya habari akizuia Chadema kufanya uzinduzi huo.

Wakati Kiswaga akitoa zuio hilo, jana Kamanda Lyanga alisema hawezi kujibu katazohilo huku akimtaka mwandishi azungumze na kaimu mkuu wa mkoa huyo.

“Siwezi kuzungumzia kauli ya mkuu wa mkoa, kama unataka mpigie yeye kwani ndiye amesema, si mimi niliyesema,” alisema.

Hata alipoambiwa kuwa utekelezaji wa agizo la katazo la Mkuu wa Mkoa utafanywa na ofisi yake, kamanda huyo alisisitiza kuwa hana cha kuzungumza na kukata simu.

Hata hivyo, Naibu Katibu Mkuu Chadema Zanzibar, Salim Mwalimu ambaye tayari yupo Simiyu kwa uzinduzi huo alisema anachokiona ni kuwepo viongozi wanaotafuta umaarufu kupitia chama chao na viongozi wake.

Mwalimu alisema ni jambo la kushangaza kuona watu wanakataza mikutano ya ndani na wengine wanaruhusu jambo linaloonesha kuwa wapo ambao wanatafuta umaarufu kupitia wao.

“Unajua kuna watu wakisikia Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa anafika mahali wanataka kutumia jina lake kutafuta uamaarufu ila sisi tunawapuuza kwani hawana jipya,” alisema.

Alisema wao wanajua taratibu zote za kufanya mikutano na wameshazifuata hivyo hawasumbuliwi na watu ambao wanatafuta umaarufu kupitia migongo yao na viongozi wao.

Mwalimu alisema ni aibu kuona viongozi wanatoa kauli za uongo bila ushahidi jambo ambalo linazalilisha nafasi zao na jamii kwa ujumla.

“Kama anasema wapeta taarifa za kuwepo kwa vurugu kwanini hawataji aliyewaambia na kuonesha ushahidi wanatupotezea muda,” alisema.

Mwalimu alisema ni vema Serikali ikafanya kazi zake kwa kufuata taratibu kwani wao hawana mpango wowote wa kuingiza nchi katika machafuko au fujo kama inavyosemwa na mkuu huyo wa mkoa.

Katika katazo lake kaimu mkuu huyo wa mkoa alisema wamepata taarifa kuwa mkutano huo wa uzinduzi operesheni kata funua utakuwa na vurugu jambo ambalo hawezi kuruhusu litokee. Alisema kupitia operesheni hiyo Chadema inatarajia kuwataka wananchi wafanye migomo hali ambayo itasimamisha shughuli za wananchi.

Kiswaga aliitaka Chadema kuacha wananchi wafanye shughuli za uzalishaji na kuachana na dhana ya kufanya maandamano kila kukicha.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo