Mbaroni akiiba lita 500 za mafuta bandarini Dar


Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imekamata mkazi wa Temeke (jina linahifadhiwa) akiwa na lita 520 za mafuta ya taa yanayodaiwa kuibwa kwenye mabomba kwenye bandari ya Dar es Salaam.

Taarifa kutoka Mamlaka hiyo zilieleza kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa hivi karibuni akiwa kwenye mtaro unaopokea maji machafu kutoka baharini, akiwa na madumu 13 yenye ujazo wa lita 40 kila moja.

“Askari wa TPA waliokuwa doria ndio waliomkamata. Mtu huyo alitoboa moja ya mabomba ya mafuta ya kampuni mbalimbali.

“Askari pia walikamata  vifaa vya uhalifu kama nyundo, tindo, bisibisi, visu, tochi ndogo 10 na mpira wa kunyonyea mafuta kutoka kwenye mabomba makubwa,” zilieleza taarifa hizo.

Zilieleza kuwa viongozi wa kampuni za usambazaji mafuta ambazo mabomba yao yamepita eneo hilo walijulishwa kuhusu wizi huo ili kuchunguza na kujua mafuta hayo ni ya kampuni ipi.

“Kwa sasa eneo husika liko chini ya uangalizi wa askari wa kikosi cha Polisi Bandari wakati uchunguzi zaidi wa tukio hili ukiendelea ili kubaini mtandao unaohusika,” taarifa zilifafanua.

Hivi karibuni Mamlaka hiyo iliimarisha ulinzi wa Bandari hiyo ikiwa ni pamoja na kufunga mitambo ya kamera (CCTV).
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Laptop City

Tangazo